free service to non-profit organisations, who cannot afford our moderate fees.

SANGO
SAME Network of
NGOs and CBOs


SANGO NI NINI?

SANGO ni kifupi cha neno la Kiingereza - yaani Same Association of Non-Governmental Organisation. Mtandao wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali yanayofanya kazi za Kimaendeleo Wilayani Same.

Katika Wilaya ya Same kumekuwepo na Mashirika kadhaa, ama yaliyoanzishwa humu Wilayani au toka nje yaliyo ya Kimataifa; yanayojishughulisha na Maendeleo. Hata kabla ya Mashirika hayo kuanzishwa ama kuingia Wilayani - yalikuwepo Mashirika ya dini - mfano Waislamu na Wakristo. Wao hawakuhubiri dini zao tu, bali walianzisha kazi mbalimbali za maendeleo, hasa Afya na Elimu na kazi nyingine za maendeleo.

Mashirika hayo, kila moja lilifanya kazi zake bila kuwa na uhusiano kati yao. Katika hali hii ndipo kukatokea watu fulani na wazo kwamba ni kwa jinsi gani Mashirika husika yanaweza kushirikiana? Na je ushirikiano huo uwe wa jinsi gani?

SANGO ikaundwa , Julai 1999, Mkutano Mkuu ukafanyika - ambao ulichagua Mwenyekiti - Bwana Dismas Nyaki, Makamu Mwenyekiti akiwa ni Bwana Mbwambo. Pamoja na viongozi hao, kulichaguliwa Halmashauri Kuu yenye watu 12. Halmashauri Kuu hufanya kazi kwa muda wa miaka mitatu.

SANGO ilisajiliwa kwenye Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi hii Januari 2000; na mwezi Machi mwaka huo huo - Mkutano Mkuu wa pili ulifanyika, wajumbe wake walikuwa ni kutoka Mashirika yaliyo wanachama. Mkutano huo uliunda Kamati ambazo ni:-


Afya
Kilimo / Mali Asili
Elimu
Jinsia
Masoko

Wajumbe wa kila Kamati hutokana na Mashirika yaliyo Wanachama - ambao kila Kamati haizidi watu kumi. Hawa hutegemea kazi wafanyazo katika Mashirika wanakotoka.

Ili kuiwezesha SANGO iwe na dira ya kazi mwaka 2000, kulifanyika warsha tena iliyoweka mkakati wa miaka mitatu. Kwenye miaka hiyo, ni kuiwezesha SANGO kuhudumia Mashirika Wanachama.

Kusudi Mashirika Wanachama yaweze kufanya kazi vizuri kwa Jamii - SANGO inapaswa kuyajengea uwezo kwa njia ya mafunzo. Pia kushawishi na kujenga mazingira mazuri huko kwenye Jamii, ambapo, Mashirika yanafanya kazi za kimaendeleo. Tena kusaidia Mashirika kuweka kumbukumbu na taarifa zao vizuri; pia kupitia taarifa na kumbukumbu kwenye Ofisi. Kutokana taarifa hizo - SANGO itaona ni wapi pa kushauri.

Kwa mujibu wa Mratibu wa SANGO - Bwana Essore Maregeri Essore alisema, "Mpango wa kwanza wa miaka 3 uliishia Desemba 2003; ukihusu kuimarisha SANGO na Sekretarieti yake kusudi iweze kuhudumia Mashirika, Wanachama wake vizuri zaidi na hata Wananchi kwa ujumla"

Kwa vile mpango wa kwanza wa miaka mitatu, uliisha mwishoni mwa mwaka (2003). Na kwamba mpango mwingine wa miaka 3 haujaandaliwa, lakini utalenga jinsi SANGO itakavyosaidia Mashirika wanachama; kusudi kwa upande wao, waweze kufanya kazi za maendeleo kwa ufanisi. Mpango utaanzia mwaka huu (2006).

Mratibu alisema "SANGO imeweka mpango wa kutembelea kila Kijiji kwenye Wilaya hii itakavyowezekana; kutoa elimu ya uraia ili Jamii itambue haki zao na ili waweze kuwajibisha Viongozi wao, kuanzia Vijijini, Wilaya hata Taifani; waonapo kuwa mambo hayaendi vizuri"

Akaongeza kuwa kazi hiyo inatarajiwa ianze katika mwaka huu wa fedha; kusudi ifikapo wakati wa uchaguzi mkuu mwakani (2006), watu wawe wameelimika vya kutosha - ili wachague viongozi bora.

Kwa kuanzia Sango ilianzisha midahalo na kushirikisha wananchi wa vijiji kutoka Kata sita katika Wilaya hii kwa majadiliano juu ya mkakati wa kuondoa umasikini na kuto fursa kwa wananchi kutoa mawazo yao juu ya mkakati wa pili unaoandaliwa na ofisi ya makamu wa Raisi.

Washiriki kwenye vikao hivyo walitoa mawazo kama walivyoona yalisaidia kuboresha, na yale yatakayosaidia siku za baadae. Kwa upande wa afya, washiriki walisema kwamba, juhudi ziongezwe kusudi kila Hospitali, Vituo vya Afya visivyo na Vyandarau vipatiwe. Na kuwe na Madaktari Watalam katika Hospitali.

Kuhusu Kilimo wanasema kwamba pembejeo zipatikane kwa wakati muafaka na kwa bei nafuu, pamoja na kupatikana kwa masoko kuwezesha Wakulima kuuza mazao yao. Hii ni mifano michache kati ya yote yaliyojitokeza Jamii iliposhirikishwa. Hivyo mawazo hayo yametumwa katika Ofisi ya Makamu wa Rais, kusudi yafahamike.

Same Association of Non-Governmental Organisation (Mtandao wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali Wilayani Same) inayo Mashirika wanachama 40. Haya Mashirika wanachama hutoa kiingilio na ada ya kila mwaka. Mashirika yamepangwa katika makundi manne kufuatana na hali ya Shirika lilivyo. Na kiingilio hata ada hutegemea hali ilivyo.

Viwango ni kama ifuatavyo:-
Wapo wanaolipa
Sh. 10,000/=
Sh. 20,000/=
Sh. 30,000/=
Sh. 40,000/=

"Pamoja na kuwa Mashirika huhitajiwa kulipa kiingilio na ada ya kila mwaka; lakini sio yote yenye uwezo. Tena kuna mengine yaliyokuwa na mawazo kwamba, kuwa mwanachama SANGO ndiyo itakayowasaidia kifedha, lakini ilipoonekana kwamba ni kinyume chake kulipa hupungua," Mratibu aliongeza

Njia nyingine za mapato ni kutoka Mashirika ya Kimataifa na ya humu nchini yasiyo ya Kiserikali na mengine yanayoshirikiana kwenye kazi - mfano VECO Tanzania. Wafadhili wengene ni PAMOJA iliyo na Ofisi Moshi, TANGO na Ofisi ya Makamu wa Rais. Kunapotokea mpango fulani wa kipekee, hutafutiwa Mfadhili ambaye mwelekeo wake hukubaliana na mradi unaokusudiwa.

ADDRESS

SAME NETWORK OF NGO/CBOs
SANGO NETWORK
P.O. BOX 108
SAME - KILIMANJARO

Tel: 027 2758097
Cell: 0744 446256
0744 580955
Email: sango_40@hotmail.com or essorem@yahoo.com

<< back

- View Guestbook
- E-mail
 
This page is still under construction:
not all links are operating

UNGANO Development Communications for all your development related communications

Kiliweb.com developed by UNGANO Ltd

In cooperation with: published yearly and costs 2.500 shillings

The Moshi Guide is published by
The Coffee Shop

 
YOUR COMPANY ON KILIWEB.COM?

send us an email
or phone : 0784-618 475
 
Updated:
10 January 2007